• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WASISITIZWA KUSHIRIKI ZOEZI LA UCHAGUZI.

Posted on: November 13th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh.Dkt Vicent Anney amewataka watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kushiriki kwenye zoezi la upigaji kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika tarehe 27/11/3024 na kuhudhuria mikutano ya kampeni za wagombea katika mitaa na vijiji wanavyo kaa.


Ameyasema hayo siku ya tarehe 13/11/2024 katika mkutano wa Baraza la madiwani uliofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda huku lengo kuu likiwa ni kujadili taarifa za robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema  ni muhimu watumishi wa umma kushiriki vyema katika zoezi la uchaguzi ili wawe mfano bora  kwa wananchi wengine huku  akiwahimiza kuwa wahamasishaji wa zoezi hilo, sambamba na hayo  ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa  ukusanyaji bora wa mapato ya ndani toka kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo na kuwahimiza kuendelea na kasi hiyo katika ukusanyaji wa mapato.

"Watumishi wengi wa umma wamekuwa na tabia ya utoro kazini hali ambayo inarudisha nyuma utendaji kazi, hivyo niwaombe kila mtu awajibike Kadri awezavyo na tuache tabia ya kupoteza mda pasipo kufanya kazi kila mtu ana takiwa kutambua wajibu wake ili tushirikiane kwa pamoja tuweze kuleta maendeleo katika Halmashauri na Wilaya ya Bunda kwa pamoja"Amesema Dkt Anney

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw.George Mbilinyi amesema  kampeni za kujinadi kwa wagombea wa ngazi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa  zitaanza tarehe 20,hadi tarehe 26 ya mwezi huu 2024 na amewaomba  Madiwani  kutumia nafasi zao kuwahamashisha wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya zoezi la upigaji kura.

"Kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika tarehe 27/11/2024 zitaanza rasmi tarehe 20 na kukamilika tarehe 26 ya mwezi huu na kama kunachangamoto yoyote kuhusu uchaguzi fika Ofisi ya uchaguzi ipo wazi na tutatatua hizo changamoto"Amesema Mkurugenzi Mtendaji.

Aidha mwakilishi wa Katibu Tawala wa mkoa wa Mara Ndugu Samson Wilium amesema kuelekea mchakato wa maandalizi ya bajeti ya fedha kwa mwaka wa fedha unaokuja ameitaka halimashauri ya Wilaya ya Bunda kutoa kipaumbele kwa miradi ya ndani ya Halmashauri kwa manufaa ya Wananchi ambayo italeta tija kwa ukamilifu wake pia amehimiza kuongeza juhudi katika kusimamia miradi yote ambayo imeanza kutekelezwa  ili ikamilike kwa wakati na ubora wa juu.

Hata hivyo Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda wameziomba baadhi ya tasisi za serikali ikiwemo Tanesco, Ruwasa na Tarura kuandaa mikakati sahihi ya kutatua changamoto ya maji, umeme na barabara ambazo zimekuwa zikiendelea kujitokeza ndani ya Halmashauri hiyo.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda