• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WILAYA YA BUNDA YAADHIMISHA MIAKA MINNE YA UONGOZI WA RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN.

Posted on: March 17th, 2025

Katika kuadhimisha miaka minne (4) ya Uongozi wa serikali ya awamu ya sita chini ya rais Dkt Samia Suluhu Hassan,Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Aswege Enock Kaminyoge, amewataka wananchi wa Wilaya ya Bunda kutoa ushirikiano wa dhati  kwa viongozi ili kufikia dhamira ya serikali ya awamu ya sita katika utoaji wa huduma za jamii.

Maadhimisho hayo yamefanyika siku ya tarehe 17/03/2025 katika ukumbi wa Malaika uliopo Bunda Mji huku lengo likiwa ni kuwafamisha wananchi juu ya shughuli na mafanikio ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita katika nyanja mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kufungua maadhimisho hayo Mh.Kaminyoge amewaagiza wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa Halmashauri na taasisi binafsi kuwatambua na kuwaheshimu viongozi wa ngazi za chini (serikali za mitaa na vijiji) ili kurahisisha utendaji kazi ikiwemo kupeleka taarifa mbalimbali kwa wananchi.

"Nawaombeni ushirikiano wa kutosha na mimi naahidi kuwapa ushirikiano unaostahili na niwakumbushe kwamba ofisi ya Mkuu wa Wilaya itakuwa wazi kusikiliza kero na changamoto za wananchi wa makundi yote na karibuni muweze kuhudimiwa"Amesema Mh Kaminyoge.

Mimi na viongozi wenzangu tunaomba ushirikiano kutoka kwenu ili kufikia adhima ya serikali ya kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na furaha katika nchi yao, pia,ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa jitihada kubwa na utendaji kazi mkubwa katika kuhakikisha inafikia malengo makubwa ya kuwahudumia wananchi wa Tanzania ikiwemo kuhakikisha wananchi wanakuwa na amani,furaha na utulivu,kuunda tume ya haki jinai, utoaji wa msaada wa kisheria pamoja na utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kwa wananchi.

Aidha,katika maadhimisho hayo, Halmashauri zote mbili pamoja na taasisi za serikali zilipata nafasi ya kuwasilisha taarifa ya matumizi ya fedha kutoka serikali kuu na wahisani kwa muda wa kipindi cha miaka minne.

Akiwasilisha taarifa ya matumizi ya fedha kwa muda wa miaka minne Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu Sai Amosi, amesema Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imefanikiwa kutekeleza shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya Elimu, ujenzi wa shule mpya za Sekondari na Msingi,kuongeza ufaulu wa wanafunzi,ulipaji wa madeni ya watumishi,upandishaji vyeo watumishi mbalimbali na uboreshaji wa sekta ya Afya.

Hata hivyo maadhimisho hayo yaliambatana na zoezi la upandaji miti katika shule ya msingi Kunzugu  iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • TIMU YA WATAALAMU WA TATHIMINI NA UFUATILIAJI WA MIRADI YA MAENDELEO WAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI

    March 27, 2025
  • MKUU WA WILAYA ATETA NA VIONGOZI WA HALMASHAURI NA WA TAASISI

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda