• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA UGANI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA KANUNI, SHERIA NA TARATIBU ZA KAZI

Posted on: November 20th, 2025

Katika kikao cha maafisa ugani kilichofanyika siku ya tarehe 20/11/2025 katika ukumbi wa Halmashauri, uliopo Kibara Stoo, wametakiwa kuhakikisha wanafanya kazi kwa kufuata kanuni, Sheria na taratibu za kazi zao.

Lengo kuu la kuitisha kikao hicho, ni kwa ajili ya kutambuana kwa watumishi wapya na waliopo, kuelezwa kanuni za kiutumishi, kupokea maagizo ya serikali, kujadili masuala ya kijamii, namna ya ukusanyaji wa mapato, kupokea taarifa kwa Kila sekta, yaani kilimo, mifugo na uvuvi.

Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ambaye ni mratibu wa zao la pamba, Ndugu.Mashaka Mashimba alisema, katika msimu wa mazao uliopita wa mwaka 2024/2025 Halmashauri ilipata jumla ya kilo 3,104,733 kutoka katika AMCOS 48 zilizopo katika Halmashauri, hivyo kupitia sekta ya kilimo iliweza kuchangia mapato ya ndani ya Halmashauri kiasi cha Tshs Milioni 113,633.227.8.

Hivyo, basi nyie maafisa ugani kwa upande wa kilimo mnalojukumu kubwa la kuwasimamia wakulima wote ili tuweze kuvuka lengo kwa mwaka 2025/2026, kuhakikisha mnatoa elimu ya kilimo cha kisasa na chenye tija, ili wakulima waweze kunufaika na mazao wanayolima.


Naye, Mwekahazina wa Halmashauri, CPA Denary Gimirey, aliwaomba na kuwasisitiza maafisa ugani hao, kuhakikisha wanashirikiana kwa pamoja katika suala zima la ukusanyaji wa mapato, kwa kuhakikisha wanaisimamia vyema minada yote iliyopo ndani ya Halmashauri inakusanya ushuru unaotakiwa, kwa upande wa uvuvi napo pamoja na sekta ya kilimo.


" Suala la ukusanyaji wa mapato ya halmashauri ni letu sote, hivyo wote kwa pamoja tunapaswa kushirikiana ili tuweze kutimiza lengo la ukusanyaji wa mapato." Alisema CPA Gimirey.


Kwa upande wa masuala ya kiutumishi, Afisa utumishi wa Halmashauri Ndugu. Modestus Chama aliwaeleza na kuwakumbusha maafisa ugani wote haki na wajibu wa Kila mtumishi pale anapokuwa kazini, ikiwemo kuhakikisha anafika kazini kwa wakati na kutimiza majukumu yake kama alivyoelekezwa na mwajiri wake, pia walielekezwa haki zao za kuomba likizo na masuala mengine ya kiutumishi.

Matangazo

  • WALIOFAULU USAILI- JIMBO LA BUNDA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO TAREHE 25/10/2025 NA 26- 27 /10/2025 KATIKA SHULE YA WASICHANA MARA October 17, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI October 11, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI October 11, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI August 27, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAAFISA UGANI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA KANUNI, SHERIA NA TARATIBU ZA KAZI

    November 20, 2025
  • CRDB BANK YAKABIDHI VITI NA MEZA KWA SHULE YA SEKONDARI MANCHIMWERU.

    November 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YANUNUA BOTI MPYA KUTOKA KAMPUNI YA FISHNET MOTORS

    November 07, 2025
  • WATUMISHI NGAZI ZA VITUO WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA FFARS ULIOBORESHWA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Istagram page
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form
  • Baraza la Madiwani

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda