• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI WATATU WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA, WAMETUNUKIWA HATI ZA PONGEZI NA HALMASHAURI KUU YA CCM

Posted on: May 24th, 2024

Katika kikao cha Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kilichofanyika katika ukumbi wa Malaika siku ya tarehe 23/5/2024, kikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama (CCM), Ndugu Mayaya A. Magesse alisema lengo la kikao hiki ni kwa ajili ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha robo ya tatu 2023/2024.

Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM, wakiwa kwenye mkutano katika ukumbi wa Malaika


Kamati ya siasa ya Wilaya ilifanya ziara ya siku tatu kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo katika majimbo yote matatu yaliyopo katika Wilaya ya Bunda na kuridhishwa na miradi yote. Pia, walimpongeza Mh. Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dkt Vicent Anney kwa ufuatiliaji na usimamizi katika miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya na kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Mh. Dkt. Vicent Anney

Aidha, katika kikao hicho Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi aliwatunuku vyeti vya pongezi watumishi watatu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kuweza kusimamia na kutekeleza ilani ya chama cha Mapinduzi kwa ufanisi katika miradi mbalimbali.

Watumishi waliotunukiwa vyeti hivyo vya pongezi ni Muhandisi wa Halmashauri Ndugu Timothy Mwanjala, kwa usimamizi wake mzuri wa miradi yote ya ujenzi inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Timothy Mwanjala, Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

Ndugu Johaness Bucha, Mratibu Mkuu na Msimamizi wa miradi ya kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, na Ndugu Roberth Nsemba ambaye ni Mwalimu kwa usimamizi wake mzuri katika ujenzi wa nyumba za watumishi Tirina, ambapo cheti chake kilipokelewa na Kaimu Afisa Elimu Sekondari Bi. Nambua Semlugu.

Ndugu. Johanes Bucha, Mratibu na Msimamizi Mkuu wa miradi ya kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Dkt Vicent Anney alisema Serikali ya awamu ya sita imetekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za Afya, Elimu, Kilimo,uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, miundombinu ya barabara, maji, usalama wa raia, uhifadhi maliasili na utulivu wa kisiasa.

 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA WANUFAIKA WA MRADI WA BCRAP

    May 15, 2025
  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda