• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KUHIMILI ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI, ILIYOPO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Posted on: May 17th, 2024

Kamati ya siasa ya Wilaya ya Bunda ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Ndugu Mayaya A. Magesse imepongeza na kuridhishwa na miradi ya kuhimili  athari za mabadiliko ya Tabianchi (BCRAP), inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda katika vijiji vya Mchigondo na Mumagunga.

Pongezi hizo zilitolewa siku ya tarehe 16/5/2024 wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua mradi wa ufugaji samaki uliopo katika kijiji cha Mchigondo, Kata ya Igundu ambapo walikagua bwawa la kufugia samaki wazazi, maabara ya kutotoleshea mayai ya samaki na vizimba vya kufugia samaki.

Mratibu wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Ndugu Johanes Bucha alisema, mbali na ufugaji wa samaki katika kijiji hicho pia wana mradi wa kilimo cha mbogamboga kwa njia ya umwagiliaji wa matone na wameshatenga eneo kwa ajili ya kilimo cha mpunga kwa njia ya umwagiliaji.

Aidha, kamati ilitembelea na kukagua mradi wa ufugaji kuku uliopo katika kijiji cha Mumagunga katika Kata ya Neruma ambapo walijionea maendeleo ya kuku hao. Mwenyekiti wa kamati ya siasa alimuagiza Mratibu wa mradi kuhakikisha anawaletea mashine ya kutotoleshea mayai ya kuku ambapo hadi sasa kuku wameshafikia hatua ya kutaga mayai.

Pia, alimuagiza Mratibu wa mradi kuhakikisha anawajengea uwezo uwezo wafugaji hao wa kuku wa namna ya kutengeneza chakula cha kuku wao wenyewe na sio kuitegemea Halmashauri pekee ili iwawezeshe kupata chakula cha kuku.

“Mradi huu unatakiwa uwe endelevu hivyo inabidi mjifunze namna bora ya kutengeneza chakula wenyewe hata mradi ukifika ukomo muweze kusimama wenyewe kwa ajili ya kujiendeleza na kukuza uchumi wenu,” Alisema Mwenyekiti wa kamati.

Wanufaika wa mradi wa kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi kutoka Mchigondo na Mumagunga waliwashukuru kamati ya siasa kwa kuja kuwatembelea na waliahidi kuiendeleza miradi yote waliyoletewa katika vijiji vyao.

Pia, walishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kuwawezesha kuwaletea miradi hiyo katika vijiji vyao kwani imewasaidia wengi na wanaendelea kujifunza kupitia wataalamu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA WANUFAIKA WA MRADI WA BCRAP

    May 15, 2025
  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda