• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YAAGIZWA KUANDAA MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI

Posted on: February 24th, 2018

Naibu Waiziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Mhe. Anjelina Mabula (MB) ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuandaa Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi. Agizo hilo limetolewa katika kikao kilichofanyika tarehe 22/2/2018 kikiwahusisha wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Mweyekiti wa Halmashauri pamoja na watumishi wa Idara ya Ardhi na Maliasili.

Akipokea taarifa ya Idara ya Ardhi na Maliasili iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw. Martine Nkwabi,  Mhe. Waziri aliweza kubaini kuwa  Halmashauri haijafanya jitihada zozote za kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi ikiwa ni pamoja na kufanya upimaji wa maeneo ya Taasisi za Serikali. Hivyo basi, Mhe. Waziri alitoa agizo alilotaka litekelezwe mara moja.  “Inasikitisha sana kuona kunakuwepo na migogoro ya ardhi katika vijiji vyetu. Kwa kiasi kikubwa migogogoro hii  inasababishwa na kutokuwepo kwa mpango wa matumizi bora ya ardhi.  Sasa ninawaagiza muandae mpango  huo angalau kwa kuhusisha vijiji 5 vyenye migogoro ya ardhi na upimaji wa maeneo ya Taasisi za Serikali uanze kufanyika  haraka iwezekanavyo”.

Pamoja na kuiagiza Halmashauri kuandaa mpango huo, pia ameutaka uongozi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa migogoro yote ya ardhi haitatuliwi ofisini. Badala yake uwekwe utaratibu wa watumishi wa ardhi kutembelea maeneo yenye migogoro ya ardhi na kutatua migogoro hiyo hukohuko kwa kuzihusisha pande zote zenye mgogoro.

Awali akitoa taarifa ya Idara ya Ardhi na Maliasili, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Bw. Martine Nkwabi alimueleza Mhe. Waziri kuwa miongoni mwa changamoto kubwa zinazoikabili Idara ya Ardhi na Maliasili ni pamoja na uhaba mkubwa wa wataalamu na Usafiri katika Kitengo cha Ardhi.  Bw. Nkwabi alibainisha kuwa  Idara inayo mahitaji ya watumishi 10 lakini mtumishi aliyepo ni 1 tu na mtumishi huyo anatarajia kustaafu kwa mujibu wa sheria mwezi Juni  mwaka 2018. Upungufu huu unachangia kwa kiasi kikubwa Idara kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa wakati na kwa  ufanisi.

Akihitimisha kikao hicho, Mhe. Waziri alikiri kupokea changamoto hizo na kuahidi kuzifanyia kazi. Aidha alisisitiza matumizi sahihi ya mfumo wa ukusanyaji wa mapato kupitia tozo mbalimbali za ardhi. Mwisho alihimiza utoaji wa hati za viwanja kwa wakati ili kuepuka malalamiko ya wananchi yasiyokuwa ya lazima kwa kumtaka Afisa Ardhi Mteule wa Wilaya ya Bunda Bw. Baraka Kambira kuhakikisha kuwa anakamilisha taratibu za upatikanaji wa hati kwa wananchi walioomba kupewa hati tangu mwaka 2016 ndani ya siku saba. Kinyume na hapo uteuzi wa Afisa Ardhi Mteule utenguliwe mara moja.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda