• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ZIARA YA KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA , KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

Posted on: October 18th, 2023

Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira iliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kukamilisha Ujenzi wa Josho la kuogeshea Mifugo lililopo katika Kijiji cha Chingurubila, Kata ya Namuhula.

Pongezi hizo zilitolewa wakati kamati ilipofanya ziara ya siku moja ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo siku ya tarehe 17/10/2023.


Miradi waliyotembelea na kukagua ni Josho la kuogeshea mifugo lililopo katika Kijiji cha Chingurubila, Kata ya Namuhula na kiwanja kilichotolewa na wananchi wa kijiji cha Mariwanda, Kata ya Hunyari kwa ajili ya ujenzi wa shule.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw. Oscar Jeremiah Nchemwa alisema, Josho hili limegharimu kiasi cha Tshs Millioni 23 kutoka serikali kuu hadi kukamilika kwake ila bado halijaanza kutumika sababu ya kusubiria uchanganywaji wa dawa kwa ajili ya kuogeshea mifugo.

Naye, Mwenyekiti wa Kijiji cha Chingurubila Bw. Bonifasi Manyonyi alisema, katika Kijiji hiki kina jumla ya kaya 101 na wafugaji 147 ambao tunategemea watanufaika na Josho hili pamoja na vijiji Jirani.

Katika ziara hiyo, wananchi wa Kijiji cha Chingurubila waliishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwapatia fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa Josho, pia waliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kuwawezesha katika Ujenzi na kuhakikisha Josho linakamilika kwa wakati.

Pia Kamati ilitembelea na kukagua Kiwanja kilichotolewa na Wanakijiji cha Mariwanda, Kata ya Hunyari kwa ajili ya Ujenzi wa shule ya Awali na msingi.

Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Mariwanda Bw. Jumanne Mwaibiro alisema, Kijiji hiki kina jumla ya vitongoji 16 na vitongoji vitatu vinapakana na Hifadhi ya Serengeti hivyo, aliiomba Kamati pamoja na Halmashauri kuwasaidia kujenga shule katika Kijiji chao kutokana na hatari ya kushambuliwa na Wanyama wakali.

Bw. Mwaibiro alisema, Kijiji hadi sasa kimeshatenga hekari 10 kwa ajili ya Ujenzi wa shule, ambapo hekari 5 tayari zimeshapimwa na hekari 5 bado hazijapimwa hivyo waliiomba Kamati kuwasaidia kupima hizo hekari 5 zilizobaki na kuwasaidia kupata hati miliki ya eneo.

“Wananchi wapo tayari kushirikiana na Halmashauri katika Ujenzi huo na kwa kuanza wameanza na usafishaji wa kiwanja.” Alisema Bw. Mwaibiro.

Kamati ilimshauri Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji kuitisha mkutano wa hadhara na Wanakijiji kwa ajili ya kujadiliana namna gani watashirikiana na Halmashauri katika Ujenzi wa shule hiyo kwa kubainisha mahitaji na  changamoto walizonazo ikiwemo ya kupata wataalamu wa kupima Ardhi ili wawasaidie kupima hizo hekari 5 ambazo hazijapimwa na kuomba Wataalamu wa Ujenzi kuwapatia ramani sahihi katika ujenzi wa madarasa hayo.

 “Wekeni juhudi sana katika suala hili la ujenzi wa shule kwa kuwataka kuwa na ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha ujenzi huo unatekelezwa na kukamilika kwa wakati ili hadi mwakani waweze kupokea wanafunzi wa Awali na msingi kwaajili ya kuanza shule”. Ilisema Kamati.

Naye, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw. Oscar Jeremiah Nchemwa alimwambia Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji baada ya mkutano huo ahakikishe anamuandikia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri muhtasari ambao utaelezea mahitaji na changamoto wanazokabiliana nazo na namna gani washirikiana na Halmashauri katika Ujenzi huo.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda