• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATU WENYE ULEMAVU HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WASISITIZWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIKOPO.

Posted on: November 7th, 2024

Afisa ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bi.Maria John amewataka watu wenye ulemavu katika kata ya Nyamanguta, Ketare na Kata ya Nyamuswa  kuunda  vikundi  ili waweze kupata mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda  itakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Ameyasema  hayo  katika ziara ya kuwatembelea watu wenye ulemavu ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda iliyofanyika siku ya tarehe 7/11/2024  huku lengo kuu likiwa ni kutoa Elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa watu walemavu na kubaini changamoto inayopelekea  watu wenye ulemavu kushindwa kujitokeza kuomba mikopo  hiyo.

Hata hivyo amesema kuwa   mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni kundi la wanawake, kundi la vijana  pamoja na kundi la watu wenye ulemavu, lakini mpaka sasa kundi la watu wenye Ulemavu hawajajitokeza kuomba mikopo hiyo.

"Mwisho wa maombi ya mikopo kwa robo ya kwanza ili kuwa  tarehe 31/10/2024 lakini watu wenye ulemavu hawajajitokeza kuomba  mikopo hiyo na pesa zenu zipo, sasa  tunatamani tufahamu  shida ni nini  hasa au hamuhitaji mikopo hiyo,na niwakumbushe  tu kuwa mkichukua mkopo  itawasaidi kujikwamua kiuchumi na kuepuka  kuwa  tegemezi"Amesema Afisa ustawi wa jamii

Kwa upande   wake   Afisa Maendeleoya Jamii Ndugu Justin Mtopwa ametoa Elimu ya namna sahihi ya kuomba  mikopo  hiyo na sifa zinazohitajika kwa waombaji  wa  mikopo hiyo,huku  akiwasisitiza  watu wenye ulemavu kujitokeza kuomba  mikopo  kwani  itawasaidia  kuinua  uchumi  wa  vikundi  na mtu mmoja mmoja.

Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye UlemavuTanzania  katika  Halmashauri  Wilaya ya Bunda Ndugu Sabasaba  Mseveni  Haji amewahimiza  watu wenye ulemavu  kujitokeza  kushiriki  uchaguzi  wa vyama  vya  watu wenye Ulemavu utakao  fanyika  tarehe 15 mwezi huu 2024 ili waweze kuchagua  viongozi  sahihi watakao  tetea  haki za watu wenye Ulemavu.

"Tunashindwa kupata haki zetu kwa sababu hatuna viongozi wanao tutetea hivyo niwaombe kujitokeza kushiriki uchaguzi  wa vyama  vya  walemavu  lakini pia tujitokeze  kugombea  na kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 ili tupate wawakilishi  sahihi watakao tusimamia vyema" Amesema Sabasaba

Hata hivyo uchaguzi wa vyama vya watu wenye Ulemavu   utafanyika  katika ngazi  ya  Halmashauri  na Wilaya na  utawahusisha  watu  wenye ulemavu wa Viungo peke yao.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda