• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAPOTOSHAJI ZOEZI LA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI "KUKIONA CHA MTEMA KUNI"

Posted on: April 25th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Mwl. Lydia Bupilipili amezindua zoezi la utoaji wa chanjo ya kujikinga na ugonjwa hatari wa Saratani ya mlango wa kizazi. Uzinduzi huo umefanyika siku ya tarehe 23/4/2018 katika Kata ya Nyamuswa ukiongozwa na kauli mbiu isemayo “Jamii iliyopata chanjo ni jamii yenye Afya. Timiza wajibu wako”

Akitoa hotuba ya uzinduzi Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka wananchi kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika  zoezi hilo ili liwe  na ufanisi kama lilivyokusudiwa ili kuiepusha jamii ya wana Bunda na ugonjwa hatari wa Saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake.

Aidha, aliwaonya wananchi kuhakikisha wanaepuka imani potofu zinazowaaminisha kuwa chanjo hiyo ina madhara kwa walengwa wa zoezi hilo. Mkuu huyo wa Wilaya aliwaonya wananchi wote wanaoeneza uvumi kuwa chanjo hiyo itasababisha ugumba kuacha mara moja tabia hiyo ya uzushi. Aliwataka wananchi kutoa ushirikianao kwa kuwafichua wale wote wanaoeneza uvumi huo ili wachukuliwe hatua stahiki za kisheria. “Serikali imejipanga kuhakikisha zeoezi hili linafanyika kwa ufanisi mkubwa, na yeyote atakayethubutu kuvuruga zoezi hili atakiona cha mtema kuni”

Mkuu huyo wa Wilaya aliendelea kusisitiza kuwa mtaji mkubwa wa mwanadamu yoyote ni afya njema ambayo itamwezesha kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi na kujiletea maendeleo bila kuathiri kipato chake kwa kugharamia matibabu makubwa ambayo angeweza kuyaepuka kwa njia ya chanjo mbalimbali zinazotolewa na Serikali tena kwa gharama kubwa.

Awali akiongea na wananchi, Diwani wa Kata ya Nyamuswa Mhe. Fyeka Sumera aliwasihi wananchi hao wa Kata ya Nyamuswa kuacha kushikilia imani potofu zinazowazuia kuwapeleka wagonjwa wao kupata huduma za kitabibu katika vituo vya afya na badala yake kuwapeleka kwa waganga wa kienyeji kwa imani kuwa wagonjwa hao wamerogwa.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Dk. Nuru Yunge aliwaasa wananchi wote kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu katika  mazoezi mbalimbali ya afya yanayofanyika ili kujikinga na maradhi mbalimbali yanayoweza kuepukwa kwa njia ya chanjo. Dk. Nuru Yunge pia alieleza kuwa sambamba na uanzishajwaji wa chanjo hiyo ya kuzuia Saratani ya mlango wa Kizazi, pia unafanyika uzinduzi wa chanjo ya Polio kwa njia ya sindano ambayo motto atapewa mara atakapofikisha umri wa wiki 14.

 Akisoma taarifa ya Hamashauri mbele ya mgeni rasmi, Mratibu wa Chanjo wa Halmashauri Bi. Magreth Nyambwa alieleza kuwa halmashauri imejipanga kutoa chanjo ya kujikinga na Saratani ya mlango wa kizazi  kwa wasichana wapatao 3932 ili kuwaepusha na athari za ugonjwa huo hatari na kuwa na jamii yenye afya itakayowawezesha kutekeleza majukumu yao ya uzalishaji mali ili kujiletea maendeleo

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda