• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wakulima na Wadau wengine wa kilimo Bunda wapata mafunzo ya kimkakati kuzuia upotevu wa Mazao

Posted on: December 17th, 2019

Wakulima na Wadau wengine wa kilimo Bunda wapata mafunzo ya kimkakati kuzuia upotevu wa Mazao

 

Na Nuru Ally, Bunda DC

KATIKA kuhakikisha wakulima wilayani Bunda,Mkoa wa Mara wanajengewa uwezo ili kuimarisha kilimo ikiwa  ni pamoja kushiriki katika kilimo cha kisasa,kuongeza uwezo wa uzalishaji,Wizara ya kilimo imeendesha mafunzo maalumu iliyowahusisha wadau mbalimbali wakilimo.

Akizungumza katika mafunzo hayo  yaliyofanyika jana katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Kibara, Bunda Afisa Kilimo Mkuu Bi. Margaret Natai kutoka wizara hiyo,alisema yameandaliwa maalum kwa ajili ya mkakati maalum wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna.

“Upotevu wa Mazao ni mkubwa, sisi wizara hatuwezi kuendelea kutazama hali hiyo ikiendelea” alisema.

Aidha,Margaret  alitaja vyanzo mbalimbali vinavyosababisha upotevu wa mazao baada ya mavuno ni pamoja na teknolojia duni za kuhifadhi mazao,ufahamu mdogo wa wadau na miundombinu duni ya usafirishaji.

Pia,alisema changamoto hiyo inatokana na ukosefu wa masoko ya uhakika,kutokuwepo kwa mitaji,uwekezaji hafifu katika tafiti na ubunifu na teknolojia duni katika uvunaji na ukaushaji.

“Wizara imeandaa mafunzo haya ikiamini kuwa mtafahamu namna ya  kudhibiti mazao ili yasipotee,’’ alisema Afisa Kilimo huyo akiongea na Wakulima na Wadau wengine wa kilimo waliohudhuria mafunzo hayo.

Awali  akizungumza katika mafunzo hayo,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Steven Ochieng  aliwapongeza  waliofanikisha kuandaliwa kwake akiamini yatakuwa msaada kwa maendeleo ya kilimo wilaya ya Bunda.

‘’Wizara ya kilimo imeleta mafunzo haya wakati mwafaka wa mavuno,’’alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji.

Bw. Ochieng alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia kulinda maendeleo ya uchumi pamoja na kusaidia wakulima kuzalisha kulingana na mahitaji.

Kwa upande wa mdau wa kilimo, Michael Kweka alisema mafunzo hayo yatasaidia kukabiliana na upotevu wa mazao na kuahidi kuwa baada ya kupokea elimu hiyo atakuwa mwalimu na mjumbe kwa Wakulima wengine juu ya utunzaji,uvunaji na usindikaji ili kuhakikisha yanawafikia walaji kwa wingi

Kupitia mafuzo haya wakulima  pamoja na wadau wengine walielimishwa juu ya athari za upotevu wa mazao baada ya kuvunwa  ikiwemo kutetereka  kwa lishe na afya ya jamii huku pia ikisababisha athari za kiuchumi.

Kabla ya mafunzo hayo baadhi ya washiriki hawakuwa na uelewa kuhusu  namna mazao yanavyoweza kupotea baada ya mavuno,lakini baada ya elimu hiyo wengi walionesha kutambua namna mazao yanavyoeza kupotea na jinsi ya kupunguza upotevu huo.

Aidha, kupitia mkusanyiko huo wadau  na wakulima kwa ujumla waliweza kuunda jukwaa la utekelezaji ambalo litasaidia kupata ushauri  na ushawishi mbalimbali ili kuhakikisha mkakati huo unatekelezeka.

Inakadiriwa kuwa kiasi cha asilimia30 hadi 40  ya mazao yanayozalishwa nchini kila mwaka hupotea kabla yakuwafikia walaji kutokana na sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ni utunzaji duni.

Ili kudhibiti hali hiyo,Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo imeamua kuandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Mazao baada ya kuvuna.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda