• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Lydia Bupilibili azindua Mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa

Posted on: July 28th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Lydia Bupilipili  amesema moja ya vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kwamba wananchi  hasa wa sekta zisizo rasmi  wanapata matibabu kupitia Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa.

Mhe. Bupilipili ameyasema hayo leo wakati wa Uzinduzi wa Mfuko wa afya ya  jamii iliyoboreshwa katika kata ya Nyamuswa Kijiji cha Nyamuswa,alieleza zaidi  kuwa Serikali  ya awamu ya Tano imehakikisha kuwa huduma ya  afya inawafikia wananchi wote haswa wenye kipato cha chini.

“Serikali ina nia ya kumfikia kila Mtanzania na kumpatia huduma bora za afya”.

Aidha Mhe Bupilipili amewataka wananchi wa Halamshauri ya Wilaya ya Bunda kuweka kiapaumbele na kuzingatia  afya zao kwakujiunga na Mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa   ili kuweza kuwasaidia pindi wanapopatwa na changamoto ya ugonjwa.

“ Natoa maelekezo na kuagiza kuwa kila  kiongozi wa kijiji kuhakikisha kaya zilizomo katika kijiji chake zinajiunga na mfuko wa ya afya ya jamii iliyoboreshwa ili kuwa na uhakika wa matibabu hata wakati hana fedha.”

“Mganga Mkuu wa Halmashauri na Mratibu wa afya ya jamii  iliyoboreshwa hakikisheni mnfanya hamasa ya kwa wananchi ili waweze kujiunga na mfuko wa ya jamii iliyoboreshwa”.

‘’Ugonjwa hauna tabia ya kutoa  taarifa kuwa  tarehe fulani utamkumba mtu fulani.unakuja  bila matarajio ya mhusika.hii ni  ni hatari kwa usalama wa mtu huyo endapo ugonjwa utamkuta hajajiunga na mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa.”amesema Mhe Bupilipili

Kwa upande wake Kaimu  mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya wilaya ya Bunda Bw.Stafa Nashon ameishukuru  serikali ya Awamu ya Tano Chini ya Dkt John Pombe Magufuli kwa kufanya mambo makubwa  katika upande wa afya kwakuweka miundombinu bora na pamoja kuanzisha kwa mfuko wa afya ya jamii  iliyoboresha.

“serikali hii imewajali wananchi na imetimiza wajibu wake wakuhakikisha jamii inapata huduma ya afya iliyobora”.alisema

 Naye, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw.Nuru Yunge  amesema kuwa huduma ya afya ya jamii gharama zimeongezeka kutoka elfu kumi hadi  elfu thelathini  lakini pia huduma zimeongezeka awali mwanachama alikuwa anatibiwa katika kituo cha afya alichojiandikishia lakini sasa hivi ukishalipia hiyo elfu Thelathini(30) utatibiwa popote ndani ya Mkoa wa Mara,hivyoUkitoa elfu Thelathini utatibiwa familia nzima ya watu sita kwa mwaka mzima katika hospitali yeyote ndani ya Mkoa.

“Lengo la Serikali ni Kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.”

Wakati huo huop,Bi.  Bhoke Makongoro Mkazi wa Kijiji cha Nyamuswa amesema mfuko  huo wa  afya ya jamii iliyoboreshwa  umesaidia mno kupunguza gharama kubwa za matibabu kwa sasa.

“sasa hivi sisi wananchi wenye kipato cha chini, si rahisi kumudu gharama za ,matibabu zinazotozwa na vituo  vya kutolea hudumu za afya.lakini ukiwa na bima ya afya jamii,hata kama fedha huna unauhakika wa kupata matibabu ya gharama yoyote”amesema Makongoro

Mfuko wa afya ya jamii ilianzishwa rasmi Mwaka 2001 ilivoanzishwa kwa sheria Mfuko wa  afya ya Jamii kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda tangu Februari mwaka huu iimeanza kutumia  mfuko wa afya ya jamii na kaya 301 zimejiandikisha na huku kaya 43458 zinategemea kujiandikisha katika mfuko huo.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda