• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Joshua Nassari ameendelea kuwaasa Wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19

Posted on: July 22nd, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Joshua Nassari amewataka Wananchi wa Bunda kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya  ugonjwa wa  Virusi vya Korona (UVIKO-19).

Mhe Nassari ametoa kauli hiyo Julai 22,2021 katika  kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri  ya Wilaya uliopo Bunda Mjini.

‘’Hatuwezi kuzui ibada zisifanyanyike,nichukue fursa hii kuendelea kuwasisitiza viongozi wa dini kuhakikisha waumini wanachukua tahadhari kwa kuhakikisha uwepo wa maji ya kunawa mikono,kuvaa barakoa pamoja na kuachiana nafasi ’’amesema Mhe.Nassari

Katika Kikao hicho Mhe Nassari alipokea Taarifa ya Tathimini ya sita ya utekelezaji wa afua za Lishe kwa Mwaka 2020-2021.

Akitoa wasilisho hilo  Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bwa. January Dalushi amesema kuwa asilimia 32 ya watoto chini ya miaka 5 Tanzania wamedumaa na hawana uwezo wa kufundishika. Kwa Wilaya ya Bunda asilimia 29 ya Watoto chini ya miaka 5 wamedumaa, asilimia 5.3 wana utapiamlo wa kadri, asilimia 0.5 ya watoto wanaozaliwa wana uzito pungufu, asilimia 4.1 wana ukondefu, aidha asilimia 3.7 ya akina mama wenye umri wa kuzaa wanaupungufu mkubwa wa damu.

Bwa Dalushi alitaja mpango mkakati  wa mwaka 2021-2022 ikiwa ni pamoja na kupanga bajeti kwaajili ya utekelezaji wa afua za lishe kiasi cha TSH,72,154,350 sawa na  Tsh.1,117 kwa kila mtoto chini ya miaka 5 kwa Bunda DC na Tsh. 27,179,351 sawa na Tsh 888.7 kwa Bunda TC, Kutoa mafunzo ya lishe, kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, kuhamasisha jamii kupitia klabu  za afya na lishe mashuleni na kufanya tathimi za lishe kila robo mwaka katika ngazi zote.

Kwa upande wake Mhe.Nassari ametoa agizo kwa Maafisa Elimu Sekondari na Msingi kuhakikisha kuwa shule zote zinaasha klabu za lishe.

‘Shule zote zianzishe klabu za lishe ili kutoa hamasa  kwa jamii na kutambua umuhimu wa lishe bora’’amesema Mhe Nassari.

Pia Mhe Nassari alipokea Taarifa ya utekelezaji wa  utoaji wa tiba kinga ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele

Akiwasilisha taarifa hiyo Dkt. Allan James alitaja walengwa wa zoezi hilo walikuwa ni  wanafunzi wote wakike na wakiume wenye umri wa miaka 5 hadi 14.

 Dkt James amebainisha idadi ya waliomeza kinga tiba  ni 61383 sawa na asilimia 84 kwa halmashauri ya Wilaya ya Bunda na 49,500  sawa na aslimia 94 kwa Halmashauri ya Mji.

Mwisho Nassari alitoa rai kwa wajumbe wa  kamati ya Afya ya Msingi kuendelea kuhamasisha wananchi kujenga vyoo pamoja na kutunza  mazingira ili kuepuka magonjwa ya  mlipuko.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda