• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe Lydia Bupilipili apokea taarifa ya Utekelezaji wa zoezi la utoaji wa Kinga Dawa ya magonjwa yalikuwa hayapewi kipaumbele.

Posted on: May 12th, 2021

Mkuu wa Wilaya  ya Bunda Mhe Lydia Bupilipili ambaye pia ni Mwenyekiti wa Afya ya Msingi (PHC) alipokea taarifa ya Utekelezaji wa Zoezi la ugawaji wa kinga  dawa kwa magonjwa yaliyokuwa  hayapewi kipaumbele.

Akizungumza wakati wa upokeaji wa taarifa hiyo wa namna zoezi la ugawaji wa kinga dawa  litakavyo tekelezwa Mei,2021 katika ukumbi wa Halmashauri ,Mhe Bupilipili alisema kabla ya  zoezi kuanza ni muhimu kuweka uelewa wa pamoja  kwa kutoa Elimu kwa jamii ili kuweza kupata ushirikiano zaidi na kuweza kupata mafanikio katika zoezi hili.

“kumekuwa na mitazamo hasi kwa jamii hasa inapotokea mazoezi  kama haya ya uotaji chanjo,ni vyema elimu ikatolewa kwa Jamii.’’

Mhe Bupilipi alitoa msisitizo kwa mratibu wa zoezi kuhakikisha kuwa watoto watakaohusika kupata kinga dawa wapate chakula kabla ya kupata dawa ili watoto hao wasije zimia au kukosa nguvu baada ya kumeza dawa.

‘Dawa hizi imeonekana zinahitaji mtoto ashibe ndio apate dawa Walimu,na jamii kwa ujumula ione umuhimu wa uwepo wa chakula wakati wa zoezi hili’.alisema Mhe Bupilipili

Kwa Upande wake Mratibu wa Afya ya Msingi (PHC)Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Dkt Allan James alitaja  magonjwa hayo kuwa ni Kichocho,Minyoo ya Tumbo,Trakoma,Matende,Mabusha pamoja na usubi yamekuwa yakiwapata watu,  kwa awali magonjwa hayo yalikuwa hayakutiliwa mkazo kama magonjwa mengine.

“Serikali kupitia Wizara ya Afya imeona umihimu wa kutoa kinga dawa kwa Magonjwa haya  sambamba na kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira ili kuepusha jamii kuathirika’.

Dkt Allan alisema kuwa zoezi la kinga dawa linakusudiwa kugawa dawa za minyoo kwa watoto kuanzia umri wa miaka mitano mpaka kumi na minne katika  shule za Msingi 104 zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

“Zoezi hili litahusisha  watoto wote walikuwa shuleni na wasiokuwa shuleni ilimradi awe katika umri wa miaka mitano mpaka kumi na minne’’alisema Dkt Allan

Mwaka 2018 zoezi la utoaji kinga dawa lilifanikiwa kwa asilimia 90 na jumla ya kiasi cha shilingi 43,044,751 kilitumika na kwa Mwaka 2021 zoezi linategemea kutumia kiasi cha shilingi 25,144,000 na linategemea kufikia jumla ya watoto 7375.

 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda