• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA, ASIKILIZA KERO NA CHANGAMOTO ZA WANAKIJIJI CHA KURUSANGA

Posted on: May 7th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Ndugu George S. Mbilinyi siku ya tarehe 4/5/2024 alifanya mkutano na wananchi wa kijiji cha Kurusanga, kilichopo Kata ya Salama katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mkurugenzi Mtendaji alisema, lengo la mkutano huu ni kusilikiza kero na changamoto mbalimbali mnazokabiliana nazo na kuona namna ya kuzitatua, leo hii nimekuja na baadhi ya wakuu wa idara kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambao nao watakuwa sehemu ya kutatua kero hizo.

Wanakijiji cha Kurusanga walimpongeza Mkurugenzi Mtendaji kwa hatua na maamuzi aliyoyafanya kwa kuja kuwatembelea na kukubali kuwasikiliza kero na changamoto zao za muda mrefu ambazo walishindwa kupata ufafanuzi na msaada kwa muda mrefu.

Wanakijiji hao walianza kwa kuomba kujengwa kwa shule ya sekondari katika eneo lililopo shule ya msingi Kurusanga, ambapo wao walisema ndio eneo ambalo lipo jirani zaidi kwa watoto wao tofauti na saivi wanavotembea umbali mrefu kufuata elimu ya sekondari katika shule ya sekondari Salama.

Pia, waliomba watengenezewe barabara katika kijiji chao kwani wamekuwa wakipata shida hasa kipindi cha mvua barabara hawana kabisa. Kero nyingine waliomba kwenye kituo cha Afya Kurusanga waongezwe wahudumu wa kutoa huduma za Afya ili kuwapunguzia mwendo wa kufuata matibabu na vipimo mbali na eneo hilo ambapo inatokana na uchache wa wataalamu katika kituo cha Afya.

Baadhi ya wanakijiji cha Kurusanga wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji katika mkutano wa Kusikiliza kero na changamoto


Ndugu Mbilinyi aliwashukuru wanakijiji hao kwa kutoa na kueleza kero na changamoto wanazokabiliana nazo na aliwaahidi kwenda kuzifanyia kazi ikiwemo suala la kuongeza wataalamu katika kituo cha Afya Kurusanga, na suala la ujenzi wa shule ya sekondari katika eneo la shule ya msingi Kurusanga aliwaambia anaenda kuunda timu ya wataalamu kutoka Halmashauri ambao watakuja kukagua eneo na kupima, na aliwaahidi atakuja kulitolea majibu baada ya taarifa kutoka kwa wataalamu hao itakapo kamilika.

Sula la matengenezo ya barabara ya Kurusanga, aliwaahidi kulifikisha sehemu husika kwani ye hana majibu nalo.

Pia, aliwashauri wanakijiji kuongeza nguvu katika ujenzi wa mabweni katika shule ya sekondari Salama, ili wanafunzi waweze kulala shuleni, huku wakisubiria kibali cha ujenzi wa sekondari mpya pale wataalamu watakaposhauri kulingana na taarifa itakavyoeleza.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda