• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA AKIFUNGA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI.

Posted on: September 29th, 2023

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bunda Bi. Changwa M. Mkwazu siku ya tarehe 28/9/2023 alifunga mafunzo kwa Watendaji wa Vijiji na kata yaliyofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katoliki lililopo Kibara.

Mafunzo hayo yalilenga kuwafundisha namna ya kutumia mfumo wa ulipaji na matumizi ya fedha za serikali katika vituo vya kutolea huduma.

Bi. Mkwazu alisema ni muhimu kuendelea kujifunza mfumo huu sababu hili ni agizo kutoka serikali kuu ya kutaka kutumia mfumo katika matumizi ya ulipaji wa fedha kutoka katika Kata na vijiji. Kikubwa itatusaidia kutuondolea usumbufu wa kuchelewa kufunga mahesabu yetu kwa mwaka, kila mmoja aende akapambane katika kufanya kazi kwa bidi ili tuweze kupata hati iliyo safi.

“Tunao uwezo wa kufanya kazi kwa bidii, niwaombe muende mkapambane na tuendelee kupeana taarifa huko kutoka katika Kata na Vijiji vyenu, ili tuweze kuzitatuta changamoto mnazo kabiliana nazo kwa pamoja. Wale ambao hamsomi mapato na matumizi kwa wananchi wenu, mjitahidi kuwasomea wanakijiji mapato na matumizi maana ni haki yao.” Alisema Bi. Mkwazu.

Mkurugenzi mtendaji aliwaomba, Watendaji wa Kata na Vijiji walete takwimu zilizo sahihi za vyanzo vyao vya mapato na mahali sahihi vilipo, pia aliwaagiza waende wakasimamie masuala ya usafi wa uchimbaji wa vyoo vilivyo bora sababu kuna mlipuko wa ugonjwa wa kuhara na tapika katika mkoa wetu.

Alisema, mwaka huu kuna uwezekano wa kuwa na mvua za Elnino, hivyo aliwaagiza kwenda kusimamia katika kusafisha mitaro huko katika mitaa wanayoishi kwa ajili ya kuepusha kuziba kwa mitaro na kupelekea milipuko ya magonjwa mbalimbali ya kutuama kwa maji machafu kipindi cha mvua.

Naye, Afisa hesabu wa halmashauri Bw. Jacob Jeconia alimwambia Mkurugenzi mtendaji mafunzo haya yamelenga matumizi sahihi ya mapato serikalini hivyo aliwaagiza Watendaji wa Kata na Vijiji wasifanye kazi nje ya mfumo huu katika manunuzi na matumizi yoyote ya ulipaji wa fedha za serikali.

“Mfumo huu umerahisisha sana katika manunuzi na namna ya kupata wazabuni mbalimbali na namna ya kuwalipa kupitia mfumo huu. Pia utawasaidia katika kuweka hesabu zao sawa na kuwapatanisha na Bank na kuwarahisishia kufunga hesabu zao za kila mwezi na kwa mwaka, pasipo kwenda Bank mara kwa mara kufuata taarifa”. Alisema Bw. Jeconia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda