• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MILA POTOFU KISIWE CHANZO CHA UKATILI WA KIJINSIA.

Posted on: November 9th, 2024

Watu wenye Ulemavu katika  kata ya Hunyari,Mugeta na kata Mihingo wamehimizwa kuachana na mila potofu ya unyanyasaji wa kijinsia ikiwemo ukeketaji kwa wanawake,kuwafungia watu wenye ulemavu majumbani na kutokuwepo  kwa  usawa  kati  ya  wanaume  na  wanawake.

Hayo yameelezwa na Afisa Ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambaye pia ni Mratibu wa watu wenye Ulemavu Bi.Maria John alipokuwa akiendelea na ziara yake siku ya tarehe 8/11/2024, ya kuwatembelea watu wenye ulemavu ndani ya Halmashauri hiyo, huku lengo kuu likiwa ni kutoa Elimu ya ukatili wa kijinsia kwa watu walemavu, Uundaji wa vikundi vya mikopo kwa watu wenye ulemavu na kushiriki katika uchaguzi wa vyama vya walemavu na serikali za mitaa.

Amesema kuwa elimu ya unyanyasaji wa kijinsia imekuwa ikitolewa kwa wingi lakini bado kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitumia mila potofu kuendeleza ukatili katika jamii zao, sambamba na hayo amewahimiza watu wenye ulemavu kuunda vikundi ili waweze kuchukua mikopo inayotolewa na halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

"Niwaombe tujitokeze kupaza sauti pindi tunapoona wenzetu wanafanyiwa ukatili ili tuweze kusaidiana sisi kama sisi na ofisi za kutoa taarifa zipo nyingi sana kuanzia wahudumu ngazi ya Afya ambao wapo katika vitongoji vyetu lakini pia tupendane na tuache kufanyiana vitendo vya kikatili, niwakumbushe tu kuwa kuna ukatili wa aina nyingi sana kama ukatili wa kimwili, ukatili wa kisaikolojia, Ukatili wa kihisia na ukatili wa kiuchumi kwahiyo niwaombe tulindane sisi kwa sisi"Amesema Bi. Maria

Kwa upande wake Mratibu wa Uibuaji wa fursa na vikwazo kwa Maendeleo wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda  Ndugu Emson Noel amewataka watu wenye ulemavu kutojishusha thamani na kutochukulia ulemavu wao kama chanzo cha kushindwa kufanya maendeleo na amewahimiza kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ili iweze kuwasaidia kukua  kiuchumi.

"Kuwa na ulemavu wa viungo siyo ulemavu wa akili na tusishinde kufanya maendeleo kisa ulemavu wetu, na waombeni sana mjitokeze kwa wingi kuchukua mikopo ambayo itasaidia kutengeneza kipato chetu wenyewe na kupunguza kuwa tegemezi katika familia zetu"Amesema Noel

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye Ulemavu Tanzania katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu Sabasaba Mseveni Haji amewahimiza wanachama wote kujitokeza kushiriki uchaguzi unaotarajia kufanyika tarehe 15/11/2024 na kusema kuwa mara ya mwisho uchaguzi huo ulifanyika mawaka 2019 na kuwataka wanachama kutumia nafasi hii kugombea na kuchagua viongozi sahihi kwa upande wao.

Hata hivyo watu wenye ulemavu katika kata hizo wamesema changamoto kubwa ya wao kushindwa kujitokeza kuomba mikopo hiyo ni ukosefu wa elimu sahihi  ya uombaji wa mikopo na changamoto ya kuandaa andiko la vikundi huku  wakimshukuru Afisa ustawi wa jamiikwa kutoa Elimu hiyo na kuhaidi kujitokeza kuomba  mikopo  katika  robo  ya pili ya  utoaji  wa  mikopo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda