• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda,Butiama ,Serengeti na Musoma Dc yanufaika na Mafunzo ya TARI

Posted on: December 5th, 2020


Pamba ni zao la nne linaloingizia Taifa kipato kwa asilimia 99 inalimwa na Wakulima wadogo na asilimia 70 mpaka asilimia 80 huuzwa nje.

Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania(TARI) kupitia kituo chake cha utafiti Ukiguru kilichopo mkoani  Mwanza  imetoa mafunzo  ya Mradi wa Cotton Victoria kwa maafisa ugani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda,Butiama,Serengeti na Musoma DC.

Akizungumza katika  mafunzo hayo kwa  maafisa ugani Bwa.Robert Ngumuo  Mtafiti kutoka TARI  amesema lengo la mafunzo hayo ni kuweka uelewa wa pamoja  yanamna yakumletea kumlima tija ili aweze kunufaika katika zao la pamba  pamoja na kuonesha umuhimu wa kufanya utafiti wa zao la pamba ili kuongeza uzalishaji kwa Mkulima.

Kwa muda mrefu zao la pamba limekuwa na teknolojia moja tu katika vipimo vya upandaji wa mbegu,teknolojia ambayo watalamu wanaeleza kuwa imepitwa na wakati.

Bw.Ngumuo ameeleza kuwa teknolojia hiyo ya vipimo iliyokuwa ikitumika katika upandaji wa mbegu ni sentimeta 90 kwa sentimenta 40(mstari na mstari sentimeta 90 pia mbegu na mbegu sentimeta 40).

“Utafiti unaonesha kuwa teknologia ya 90 kwa 40 imetumika kwa muda mrefu lakini bado haijamkomboa mkulima”.alisema Ngumuo utafiti

Ngumuo anasema kuwa teknologia ambazo wanazifanyia utafiti ilikuleta kwa wakulima,zitaweza kuwaomboa wakulima na kupunguza gharama za uzalishaji

Ngumuo anazitaja teknologia hizo mpya ambazo TARI inazifanyia  utafiti kuwa ni sentimeta 50 kwa sentimenta 30,(mstari na mstari 50,mbegu na mbegu sentimeta 30),sentimeta 60 kwa 30.

Nyingine ni vipimo vya  sentimenta 70 kwa 30 pamoja na sentimeta 80 kwa 30

‘Vipimo hivyo vinaweza kubadilika vikawa sentimenta 50 kwa 16.67,60 kwa 16.67,70  kwa 16.67 pamoja na 80 kwa 16.67.”alisema Ngumuo

Aidha Ngumuo anaeleza kuwa  kwenye teknologia zote hizo,lengo lake kubwa ni kuongeza mazao shambani,kwani matumizi ya teknologia ya zamani 90 kwa 40 imekua ikiacha nafasi kubwa kufanya  mkulima kutonufaika kutokana na kupata mazao machache.

“teknologia hii inongeza mavuno yanakuwa mengi kwa sababu kunakuwa na miche mingi ya pamba katika eneo dogo”.alisema Ngumuo

Naye, Dkt Paul Saidia Mtafiti kutoka TARI Ukiguru anasema kuwa kuwa teknologia hizo mpya,suala,la mbolea ni muhimu sana kwani uchaguzi mzuri wa mbolea hufanya mazao yakue kwa ustawi mzuri zaidi.

Dkt Saidia anaeleza zaidi kuwa utumiaji wa mbolea za kisasa,ikiwemo urea na mbolea yakukuzia mmea uweze kuwa na afya nzuri na kuzaa matunda ya kutosha.

“Kwa kutumia mbolea kila mche mmoja wa pamba unatakiwa kuwa na  vitumba kuanzia 20 na kwenda juu,lakini ukifanya vizuri na kuzingatia kanuni zote mche unaeza kubeba vitunda hadi 40  hata mbolea ya samadi ni sahihi kwa matumizi”. Anasema Dkt Saidia

Benson Mturi Afisa kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda alisema amefurahia elimu  hiyo iliyotolewa na  hivyo itawasaidia kuwafundisha wakulima upandaji mzuri  wa mbegu za pamba kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazoelekezwa katika kilimo cha pamba.

“kupitia mafunzo haya yaliyotolewa na TARI naamini sisi ndio tutakuwa mabalozi wazuri kwa Wakulima wetu.”alisema Mturi

Kwa upande wake Bwa. Ruge Kelvin Afisa Kilimo Mkoa wa Mara  Ametoa wito kwa  Maafisa kilimo wote walioshiriki katka mafunzo haya  kuzingatia maelekezo yaliyotolewa pamoja na kuyafanyaia kazi`           

“ kila Halmashauri ikawe mfano wa  kuigwa kupitia mafunzo haya naomba tusiangushane”Anasema

Bwa. Kelvin amewapongeza na kuwashukuru TARI kwakuendelea kuwa bega kwa bega na  Wakulima kwa kuendelea kutoa Elimu ambayo inatija kwa Mkulima.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda