• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YAWAPA MAFUNZO WAHUDUMU WA AFYA KATIKA NGAZI YA VIJIJI

Posted on: October 12th, 2023

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Daktari Hamidu Adinani alifungua mafunzo ya siku mbili kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Vijiji yaliyofanyika katika Shule ya Sekondari Mwibara siku ya tarehe 5/10/2023.

Daktari Adinani alisema, lengo la mafunzo haya ni kuwawezesha Wahudumu wa Afya ngazi ya Vijiji kuwatambua watu wenye Lishe duni katika Jamii, ambao inapelekea kupata Utapiamlo na Udumavu kwa Watoto walio chini ya miaka Mitano (5).

“Tunawapa mafunzo haya ili muweze kuwatambua kina Mama Wajawazito, Watoto na Wazee wenye changamoto ya Lishe katika Vijiji na kuwasaidia katika kuwaelimisha namna bora ya kuweza kuandaa chakula chenye mchanganyiko wa Lishe yenye virutubisho sahihi kwa kufuata makundi muhimu ya vyakula ili kuepusha kupata Utapiamlo na Udumavu kwa Watoto.” Alisema Daktari Adinani.

Kaimu Mganga Mkuu aliwaagiza kwenda kufanya kazi kwa bidii kwa kushirikiana na Wataalamu waliopo katika Zahanati pamoja na Hospitali zilizopo katika Kata na Vijiji, ili kumuhaisha mtu mwenye changamoto ya Utapiamlo mara tu watakapomtambua mapema.

Alisema ili kuondokana na  zana potofu za imani za Kishirikina katika Vijiji na Kata zetu mnatakiwa mkawaelimishe kwenda kwenye vituo vya Afya mara tu wanapoona mtu ana changamoto za Lishe duni. Kwa kumshauri kwenda kwenye vituo vya Afya kwaajili ya kuonana na Wataalamu.

Pia aliwaomba kutoa ushirikiano kwa kina Mama Wajawazito kwa kuwashauri na kuwaelimisha umuhimu wa kuhudhuria Kliniki mara tu wanapojihisi kuwa ni Wajawazito na sio kusubiria hadi miezi mitatu ndio aanze kuhudhuria Kliniki, hii itaepusha kupata madhara wakati wa kujifungua na wakati mwingine kuepusha vifo vya Mama na Mtoto maana watashauriwa vyema na Wataalamu waliopo katika vituo vya Afya jinsi ya kuandaa Lishe iliyo bora hadi atakapojifungua salama.

Daktari Adinani alisema, mmekuwa msaada mkubwa sana kwenye sekta hii ya Afya kwa ngazi ya Vijiji, ni matarajio makubwa kwa Halmashauri ya Wilaya kwamba, baada ya mafunzo haya mtaenda kuyafanyia kazi kwa kushirikiana vyema na Wataalamu waliopo katika Zahanati na Hospitali zetu huko katika Kata na Vijiji kwa kuwatambua mapema wale wote wenye viashiria vya hatari kwa kuhakikisha mnawawahisha  katika vituo vya Afya mapema.

Naye, Mkufunzi wa mafunzo hayo ambaye ni Afisa Lishe wa Mkoa wa Mara Bw. Benson Sanga alisema lengo la mafunzo haya ni kutambua majukumu yenu katika Vijiji kwa kuhakikisha mnafuatilia matibabu ya Utapiamlo mara tu mnapohisi mtu amepata changamoto kwa kuhakikisha anafika katika kituo cha Afya mapema na kupatiwa matibabu.

Pia walifundishwa, namna ya kupima hali ya Lishe kwa Watoto wote kuanzia umri wa miezi 6 hadi miaka 5 ili kuweza kutambua hali ya udumavu kwa Mtoto ambaye amekosa Lishe iliyo bora.

Pia walifundisha namna ya kutoa elimu kwa Mama Mjamzito kwa kuhakikisha anahudhuria Kliniki mapema na kwa wakati kwa kula Lishe iliyokamili kwa kufuata makundi sahihi katika kuandaa Lishe.

Mafunzo hayo yalihudhuriwa na Wahudumu wa Afya ngazi ya Vijiji 96 kutoka katika Vijiji 48 na Kata 12 za Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda