• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yatoa motisha kwa Shule ,Walimu na Wanafunzi waloffanya vizuri matokeo ya darasa la saba mwaka 2020

Posted on: February 20th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imetoa motisha kwa walimu,wanafunzi  pamoja na shule zilizofanya vizuri katika Nyanja mbalimbali kwa mwaka 2020.Ambapo tunzo hizo zilijikita katika  utunzaji mazingira,Taaluma, uendeshaji wa miradi pamoja na madarasa yanayongea.

Akizunguza  katika  hafla ya utoaji tuzo iliyofanyika katika ukumbi wa kanisa  la Kibara  Februari 18,2021 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bunda Bwa. Amos Kusaja alisema  Idara ya Elimu msingi ni idara inayoongea,katika idara zangu zote za halmashauri ya Wilaya ya Bunda elimu msingi inafanya kazi.

“Nampongeza Afisa Elimu Msingi pamoja na timu mzima kwakuendelea kuifanya halmashauri ya wilaya bunda kung’aa kimkoa kwakushika nafasi ya tatu”.alisema Bwa. Kusaja

Aidha  Bwa Kusaja ameeleza kuwa  bajeti ya 2020/2021 imetengwa milioni mia moja kutoka mapato ya ndani  kwaajili ya ujenzi wa madarasa shule za msingi.

Kwa hatua ingine Bwa Kusaja alitoa shukrani kwa  Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa  na Mhe  Dkt John Pombe Magufuli  kwakuendelea kupunguza changamoto katika Elimu , wadau wa elimu PCI kwa kuendelea kutoa mafunzo kwa walimu wa KKK,Project Zawadi na NMB bank kwakuendele kuchangia katika ujenzi wa madarasa

“Niwashukuru NMB bank kwasababu wametuahidi kutuunga mkono na mwaka huu wametuhadi watatupa shilingi  milioni  10 kwaajili ya ujenzi wa madarasa’.alisema Kusaja

Naye Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya Bunda Mhe Lydia Bupilipili alisema katika elimu  motisha ni kitu kizuri

“Binadamu yeyote katika kufanya kazi anapenda kupata motisha’.alisema mhe Bupilipili

Aidha Bupilipili amewataka walimu kuongeza juhudi katika kutekeleza majukumu yao kwani  hiyo ni moja ya nguzo  ya kuimarisha  ufaulu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

‘panapo kuwa na kwanza na mwisho yupo ninaimani kwa juhudi hizi ufaulu utaongezeka zaidi’.alisema Bupilipili

Mhe Bupilipili aliongeza kusema kuwa  kila mmoja ana wajibu wakufanya kazi, na tuongeze juhudi sababu inawezekana kabisa kushika nafasi ya kwanza kimkoa.

Kwa hatua inginge mhe Bupilipili ametowa wito kwa wananchi kuendelea kuwaheshimu walimu ili kuendelea kuleta ushirikiano bora baina ya mwalimu na mwanafunzi.

“Wapo baadhi ya wananchi anapoana Mwanafunzi akiadhibiwa wao wanahukumu mwalimu,waache hiyo tabia mara moja’.alisema Bupilipili

Kwa pande wake Afisa Elimu msingi Bwa. Reginald Richard ametaja mikakati ya  idara ya elimu msingi ni kupandisha  ufaulu  wa darasa la nne kuwa ni 100% na darasa la saba ni 95% kwani dalili za kufikia malengo  haya yamewezekana,kudhibiti utoro kwa  walimu na wanafunzi,kumaliza tatizo la KKK na  kuboresha kamati za maendeleo ya elimu kata.

Bwa. Richard aliwataka walimu kuendelea kutekeleza majukumu yao kiufanisi pamoja na fuata taratibu za ufundishaji ili kuweza kupata matokeo mazuri zaidi.

‘Ushirikiano baina yetu ndio utatufanya tusonge mbele zaidi”alisema Bwa. Richard

Aidha Bw. Richard ametoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya Tano kwakuendelea kumaliza changamoto mbalimbali katika elimu na kutengeneza mazingira bora ya kufundisha na kujifunza.

‘kwakweli mpaka tunaishukuru serikali maana mazingira ya shule zetu yanavutia kwa asilimia kubwa’

Naye ,Mwalimu Malindi Majige kutoka shule ya Msingi Mwibara alitoa shukrani kwa niaba ya walimu wengine alitoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya tano kwakuendelea kuangalia masilahi yao pamoja na wadau wengine.

‘sisi kama walimu tunafarijika na tunapata hamasa yakufanya vizuri zaidi’.

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina jumla ya Tarafa tatu ambazo ni Chamriho,Kenkobyo na Nansimo, ina jumala ya kata 19 na Shule za msingi 104 kati ya hizo shule 100 ni za serikali na 3 na watu binafsi na 1 inamilikiwa na kanisa.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda