• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZEE WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA KATA, VIJIJI NA VITONGOJI ILI WAWEZE KUTAMBULIWA

Posted on: October 1st, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda imeadhimisha siku ya wazee duniani ambapo maadhimisho hayo yamefanyika katika Kata ya Hunyari siku ya tarehe 1/10/2024, na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Ndugu Noel Shamazugu.


Ndugu Shamazugu aliwashukuru wazee wote waliojitekeza katika madhimisho hayo ambapo alisema lengo kuu la kuadhimisha siku hii ni kwa ajili ya kuongeza uelewa katika jamii kuhusu masuala mbalimbali ya wazee ikiwa ni Pamoja na kutafakari fursa na changamito zinazowakabili wazee na kuona ni namna gani wataweza kuzitatua changamoto hizo.

“Katika kutimiza adhima ya wazee kwa kuwafanya waishi Maisha mazuri na kuwapa huduma nzuri, serikali ipo katika hatua za mwisho za kuboresha sera za wazee kwa kuona ni namna gani watazitatua changamoto zao.” Alisema Ndugu Shamazugu.

Alisema, mikakati ya serikali ni kuendelea kufanya utambuzi wa wazee wote waliopo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ambapo kwa mwaka huu 2024 jumla ya wazee 6302 tayari wameshatambuliwa hivyo, watapatiwa vitambulisho vya msamaha wa matibabu. Serikali imeendelea kuwaunganisha wazee na mfuko wa TASAF ili waweze kujiendesha maisha yao wenyewe pasipo kuwa tegemezi katika jamii.


“Tunaamini kupitia mfuko huu wa TASAF ambao huwa unatolewa kwa walengwa kwa kipindi cha miaka mitano mzee utakuwa umeshajipanga vizuri kwa kuanzisha mradi hata wa ufugaji mbuzi ambao watakusaidia katika kuendesha maisha, miaka mitano inapoisha huwa wanawaondoa walengwa wa awamu ya kwanza na kuwekwa wengine. Hivyo mzee unapopata fursa hii ya kuingia kwenye mfuko wa TASAF unatakiwa zile fedha unazozipata uanze kufikiria mradi wa kufanya na sio kula tu maana miaka mitano inapoisha serikali inaamini utakuwa umesogea kwa sehemu Fulani.” Alisema Kaimu Mkurugenzi.

Halmashauri tunaendelea kupokea na kufanyia kazi malalamiko na changamoto mnazokabiliana nazo kupitia serikali za vijiji na vitongoji kwa kuhakikisha tunaboresha na kutatua changamoto hizo, tunaendelea kuboresha na kuanzisha madirisha ya wazee katika vituo vya Afya na hospitali zetu, ili mzee unapoenda kupata huduma uhudumiwe kwa haraka na sio kupanga foleni muda mrefu kusubiria.


Katika kuadhimisha siku ya Wazee duniani huduma mbalimbali ziliweza kutolewa ikiwemo ugawaji wa dawa bure, upimaji wa Afya, ugawaji wa vitambulisho vya msamaha vya matibabu na upimaji wa hali ya Lishe.

Naye Afisa Ustawi ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Bi. Fausta Gabriel alitoa elimu mbalimbali kwa wazee kuhusiana na ukatili wa wazee, haki za wazee, elimu ya bima ya Afya ya iCHF na elimu kuhusu haki za wazee kwa mujibu wa sera yam waka 2003.


Katika maadhimisho hayo Halmashauri iliweza kuzindua Program Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa ngazi ya Kata.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda