• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WA HAMASISHWA KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

Posted on: November 24th, 2024

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Ndugu Salum Khalfan Mtelela ameziagiza taasisi za Serikali ndani ya Wilaya ya Bunda kuhakikisha wanafata maelekezo ya kutumia nishati safi ya kupikia kabla ya tarehe elekezi iliyotolewa na Raisi wa Tanzania kwa taasisi za Serikali kuanza kuumia nishati hiyo ili kulinda mazingira na kuunga mkono kampeni ya Raisi Samia Suluhu Hassan ya matumizi  Safi ya nishati ya kupikia.

Ameyasema hayo katika kilele cha mashindano ya Upandaji Miti katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yaliyo fanyika katika Shule ya Msingi Mwibara siku ya tarehe 24/11/2024.




“Nitumie nafasi hii kuwakubusha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kujitokeza kwa wingi siku ya tarehe 27/11/2024 ili kupiga kura na kuchagua viongozi ambao ni sahihi na wataleta maendeleo katika Halmashauri na Wilaya kwa ujumla na pia kushiriki mikutano ya kampeni za wagombea ilikubaini kiongozi yupi ni sahihi kwa upande wenu”Amesema Ndugu Mtelela

Katika  mashindano hayo kulikuwa na michezo mbalimbali kama kukimbiza kuku, kuruka kamba, Mpira wa miguu pamoja na mazoezi ya viungo  na washindi wa michezo hiyo walipewa zawadi mbalimbali.




Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bw.George S. Mbilinyi amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuunga Mkono Kampeni ya matumizi safi ya Nishati ya kupikia na utunzaji wa mazingira pamoja na kuhamasisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unao tarajia kufanyika tarehe 27/11/2024.

"Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ipo vijijini na wananchi wengi wanategemea kuni pamoja na mkaa kwaajili ya kupikia  hali inayo pelekea uharibifu wa mazingira, kwahiyo tumeamua kutoa Elimu hii kwa wananchi ili waweze kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na kuanza kutumia nishati Safi ya kupikia  (GESI)"Amesema Mkurugenzi Mtendaji



Kwa upande wake Afisa kilimo na mratibu wa Mradi wa kuhimili Athari za mabadiliko ya tabia ya nchi  (BCRAP)  Ndugu, Johanes Bucha amesema mpaka sasa wamefanikiwa kupanda zaidi ya miti ya mbao15,218  na miti ya matunda mbalimbali ikiwemo maembe 500, mapera zaidi ya 3000 na parachichi zaidi ya 1000.

"Katika zoezi letu la upandaji wa miti tumekutana na changamoto ya mifugo holela ambayo imekuwa ikiharibu sana miche tunayopanda kwahiyo tunaomba ngazi za vijiji kuweka sheria kwa wafugaji holela na niwaombe wananchi kuendelea kumwagilia miti tunayopanda ili iweze kusitawi vizuri"Amesema Bucha.

Afisa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Ndugu, Moshi Ngombolwa amesema matumizi ya nishati isiyo Safi ya kupikia ni pamoja na kutumia mda mrefu wakati wa kupika na macho kuwa mekundu hali inayopelekea baadhi ya maeneo kuhusisha na Imani za kishirikina.

"Tunashauri wananchi kuwa makini sana katika suala zima la utunzaji wa mazingira kwahiyo tunashauri jamii ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuanza kutumia nishati Safi ya kupikia (GESI) ili kuendana na kampeni ya Rais wa Tanzania na kutunza mazingira kwa kutokukata miti kwajili ya kuchoma mkaa na kuni za kupikia"Amesema Afisa Mazingira.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda