• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA BUNDA WAFANYA KIKAO CHA KWANZA NA WADAU WA SEKTA YA MAJI

Posted on: October 7th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Joshua Nassari amezitaka Jumuiya za watumiaji maji Wilaya ya Bunda kusimamia ipasavyo miradi ya maji iliyo katika maeneo yao, kwa kuhakikisha kuwa  fedha zinazokusanywa zinatumika vizuri ikiwemo na kulipia bili ya maji kila Mwezi.

Hayo amesema leo Oktoba 7,2021 katika Mkutano wa  kwanza wa Wadau wa Sekta ya Maji Wilaya ya Bunda uliosimamiwa na  Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijiji(RUWASA) uliofanyika katika ukumbi wa Malaika uliopo Bunda Mjini.

‘’Sisi kama wadau ,kama viongozi ni lazima tuhimize wananchi walipie huduma ya maji ili kuepusha usumbufu wakukatiwa maji’’amesema Nassari

Aidha Mhe Nassari  amesema kuwa   fedha zote zinazokusanywa na jumuiya ya maji kutoka kwa Wananchi wa eneo husika zinatakiwa kubaki ili kutanua mtandao wa maji katika maeneo hayo sambamba na hilo kuhakikisha miundombinu inatunzwa na kuthaminiwa ili kuepusha manunuzi na marekebisho ya miundombinu.

‘’serikali inahakikisha kuwa kila mwananchi anafunga maji nyumbani,katika juhudi za kupambana Kumtua ndoo mama kichwani’’amesema Mhe.Nassari

 Naye,muwakilishi wa meneja wa RUWASA mkoa wa Mara afisa utumishi  Stanley Sing’ira  amebainisha kuwa lengo la RUWASA ni kuhakikisha Mamlaka hiyo inatoa huduma ya maji kwa wananchi huku akiendelea kusisitiza jumuiya za maji  kuendelea kusimamia miradi ya maji ili iwe endelevu.

‘’Maji ni muhimu katika shughuli zetu za kila siku ni jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha maji yanapatikana kwa kila mwananchi na kwa wakati’’amesema Sing’ira

Kwa upande wake meneja wa RUWASA wilaya ya Bunda  Eng. Lukas Madaha amekemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya watu vya kuhujumu miundombinu ya maji kwani kwakufanya hivyo ni kinyume na taratibu za sheria na atakae bainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa  sheria.

‘’kumekuwa na tabia ya baadhi ya wananchi kuharibu pamoja nakuchukua vifaa na kupelekea huduma katika eneo husika kupotea,hivyo niwaombea wadau tuwasisitize wananchi kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzake katika kulinda miundombinu ya maji’amesema Eng. Madaha

Mkutano huo uliambatana na mada mbalimbali zikiwemo Mada migogoro katika kamati za maji,utaratibu wakuunda vyombo vya watumiaji maji ngazi ya jamii na uendeshaji wake,programmu nzima ya Maji na Upangaji bei maji.Sambamba na mada zilizotolewa aidha wajumbe walipata nafasi ya kujadili na kupata maazimio ya mkutano wa kwanza  wa Mwaka wa Wadau wa Sekta ya Maji.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda