• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA MARA AWATAKA WAKANDARASI KUWA WAADILIFU

Posted on: January 5th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mh. Said M. Mtanda siku ya tarehe 4/1/2024 amefanya mkutano na Wakandarasi wote wanaojenga katika shule ya sekondari ya Mkoa ya wasichana, iliyopo katika kijiji cha Bulamba, kata ya Butimba, katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mbali na mkutano huo Mh. Mkuu wa Mkoa alitembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo, kwa kukagua jengo moja baada ya lingine, ili kuona maendeleo ya mradi huo ulipofikia.

Mh. Mtanda aliwaambia wakandarasi hao lengo la ziara yake ni kwaajili ya kuona maendeleo ya mradi huo wa ujenzi ulipofikia, na kuwasisitiza kuongeza kasi zaidi katika kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kwa wakati.

Pia, aliwaambia anatarajia kuja kuupokea mradi huo mwishoni mwa mwezi wa Kwanza hivyo aliwataka wakandarasi wote kuhakikisha wanaukabidhi mradi kwa tarehe husika.

“Tunataka Wakandarasi waadilifu katika mradi huu ambao wanafanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanakamilisha kwa wakati. Mradi kama huu unatekelezwa Kitaifa katika mikoa 16 na Halmashauri hii ni mojawapo katika kutekeleza mradi huu wa ujenzi wa shule ya Mkoa ya wasichana, hasahasa katika Kijiji hiki cha Bulamba, Kata ya Butimba, Tuishukuru serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mh. Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha kutupatia kiasi cha Tshs Bilion 4 katika mradi huu.” Alisema Mh. Mtanda.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa aliwaambia hatamvumilia mtu yeyote yule mwenye nia ya kuhujumu mradi huu, hivyo aliwataka kufanya kazi kwa uadilifu na kwa uaminifu ili kuhakikisha mradi unakamilika na kuukabidhi kwa wakati sahihi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda