• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUTANO WA WAZAZI NA KAMATI YA MAENDELEO YA SHULE, KATA YA IRAMBA

Posted on: January 18th, 2024

Diwani wa Kata ya Iramba, ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Mh. Charles Manumbu siku ya tarehe 17/1/2024 amefanya kikao na Wananchi wa Kata ya Iramba, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mkutano huo ulifanyika katika shule ya Sekondari Kwiramba baina ya Wazazi/Walezi, Kamati ya shule pamoja na Wanafunzi, lengo likiwa ni kuangalia na kutathimini maendeleo ya Elimu katika Kata hiyo.

Mh. Manumbu alisema nimeona ni muhimu tukiwa ni Wazazi na  Walezi wa Wanafunzi wetu tukutane, tujadiliane, tuelezane na tufanye maazimio ambayo ni lazima tuyazingatie na tuyatekeleze ili kuweza kuinua kiwango cha ufaulu kwa Wanafunzi katika Kata hii. Kufanya tathimini ya miaka mitatu kwa matokeo ya darasa la Nne, la Saba, kidato cha Pili na cha Nne.

Walimu wa shule za Msingi na Sekondari waliweza kuwasilisha taarifa zao za matokeo kwa madarasa hayo kwa kipindi cha miaka mitatu, kwa kueleza changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo Wanafunzi hao hadi kupelekea ufaulu mdogo katika Kata hiyo.

Wazazi/walezi, nao walipata wasaa wakuchangia katika mkutano huo, hivyo, walijadiliana kwa pamoja kuona ni namna gani wanaweza kuzitatua changamoto hizo zilizotajwa na Walimu hao ambazo ni umbali wa kutoka nyumbani hadi shuleni, uhaba wa Walimu katika shule ya Kwiramba, pamoja na utoro sugu.


Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Kwiramba, Bwana Fiti Mjalifu aliwataka Wazazi na Walezi kujitathimini katika masuala ya Elimu kwa Watoto  wao kwa kuhakikisha wanawahimiza kufika shuleni kwa wakati na kuhudhuria vipindi shuleni kwa kuhakikisha kila siku wanakagua madaftari yao, pia aliwataka kuwafundisha Watoto wao maadili yaliyo mema na sio kuwategemea Walimu peke yao kwenye suala na nidhamu.

“Wazazi na Walezi tukizingatia haya itasadia kupunguza utoro sugu kwa Wanafunzi na kuwafanya kuwa na maadili yaliyo mema, hivyo itachangia kuongeza kukuza ufaulu kwa Wanafunzi katika shule hii ya Sekondari.” Alisema Bw. Mjalifu.

Wazazi na Walezi waliomba Walimu wa masomo katika Sekondari ya Kwiramba waongezwe, pamoja na kujengewa mabweni kwa Watoto wa kike hasa wa kidato cha Pili na cha Nne.

Naye, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Ndugu Wandere Lwakatare aliwaahidi Wazazi na Walezi kumleta Mhandisi wa Halmashauri kwa ajili ya kuja kuangalia na kushauri kuhusiana na baadhi ya majengo yaliyopo shuleni hapo kama yatatafaa kukarabatiwa  kwa matumizi ya mabweni ya Wasichana hasa kwa kidato cha Pili na cha Nne.

Ndugu Lwakatare, aliwasisitiza Walimu kupenda kutumia lugha ya Kiingereza mara kwa mara ili Wanafunzi waweze kuijua na kuizoea kuitumia ambapo itawasaidia katika kuelewa masomo yao na kuwasaidia kufanya vizuri katika mitihani hayo, sababu masomo yote yanafundishwa kwa lugha ya  Kiingereza.

Suala la kuongezewa Walimu katika shule hiyo, Ndugu Lwakatare aliwaahidi kulichukua na kulifikisha sehemu husika ambao ndio wanaowapangia Walimu vituo vya kazi. 

Katika mkutano huo viongozi wa Serikali, Wazazi na Walezi waliazimia mambo yafuatayo, ambayo ni Wazazi na Walezi kuhakikisha wanakuja shuleni mara kwa mara kwa ajili ya kufuatilia maendeleo ya Watoto wao na kuhakikisha wanawahimiza kudhuria vipindi vyote shule kwa kuhakikisha wanakagua madaftari yao kila siku, kuhakikisha wanachangia Lishe shuleni, ili Watoto waweze kula chakula shuleni.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Wananchi kutoka vijiji vitano vilivyopo katika Kata  ya Iramba, ambavyo ni Isanju, Sikiro, Mwiruruma, Mgala na Nyalugoma.

        

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda