• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA YAPOKEA JUMLA YA VITABU 60,739 KWA SHULE ZA AWALI NA MSINGI, PAMOJA NA SEKONDARI

Posted on: November 13th, 2023

 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ilipokea vitabu vya Kiada na Hadithi kwa shule za Sekondari na shule za Awali na Msingi kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), ambapo jumla ya vitabu 371 kwa shule za Sekondari vilipokelewa, na 60,368 kwa shule za Awali na Msingi.


Zoezi la ugawaji wa vitabu lilifanyika siku ya tarehe 10/11/2023 katika shule ya Sekondari Mwibara, iliyopo Kibara Stoo, na jumla ya shule 124 zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ziliweza kugawiwa vitabu hivyo.

Kaimu Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Bw. Phinius Ouko alisema jumla ya shule 17 za Sekondari ziligawiwa vitabu vya mchepuo wa Sayansi ambapo kidato cha Nne walipata vitabu 158 kwa somo la Fizikia na Kemia vitabu 126, kwa kidato cha Tatu waligawiwa vitabu 87 kwa somo la Fizikia. Na kwa shule za Awali na Msingi 107, nao waliweza kugawa vitabu 32,240 vya Kiada na vitabu 28,128 vya Hadithi.


“Tunamshukuru sana Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kuletewa vitabu hivi katika Halmashauri yetu, kwani kupitia vitabu hivi hasa vya madarasa ya Awali na msingi tutapunguza zile KKK mashuleni kwa watoto wetu na kwa upande wa shule za sekondari vitabu hivi vitaongeza motisha kwa walimu na wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi”. Alisema Kaimu Afisa Elimu.

Bw. Ouko alisema, tunaiomba serikali pia, ituletee vitabu vya mchepuo wa Kiingereza kwa shule za Awali na Msingi, kwani katika Halmashauri yetu tuna shule ya mchepuo wa Kiingereza ambayo ni Bunda English Medium. Pia tunaomba kuwe na uwiano wa kila mwanafunzi mmoja na kitabu chake shuleni kwa kila somo.

Naye, Mwalimu Zaituni Semvua wa shule ya Msingi Mariwanda A, alisema, anamshukuru Mh. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwaletea vitabu hivi na aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kupitia Mkurugenzi Mtendaji kwa  kufanikisha zoezi hili la ugawaji wa vitabu.

“Zoezi la ugawaji wa vitabu linaenda kuziba sehemu ya mapungufu wa vitabu, ambapo hapo awali kitabu kimoja walikuwa wanatumia wanafunzi Wanne hadi Watano hivyo kupelekea ugumu kwa mwanafunzi kuelewa. Tunashukuru kwa vitabu vya darasa la Nne na la Tano tumeletewa vingi na kwa darasa la Awali hadi la Pili kwa hivi vitabu vya Hadithi vinaenda kupunguza uwingi wa Wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika.” Alisema Mwalimu Semvua.

Naye, Mwalimu wa shule ya Sekondari Mwibara, ambaye ni Mkutubi Bw. Ludonya Lucas alisema,  zoezi hili ni zuri kwa serikali na Halmashauri yetu, hivyo aliomba wanapokuwa wanaleta vitabu na kuvigawa wawe wanaleta vitabu vya masomo yote na kwa vidato vyote kuanzia kidato cha Kwanza hadi cha Nne.

“Vitabu hivi vitasaidia kupunguza uhaba tuliokuwa nao hapa shuleni, maana vitabu vya Fizikia na Kemia tulikuwa navyo vichache sana na havitoshelezi” . Alisema Mwalimu Lucas.

Walimu wa shule za Msingi na Sekondari walipongeza zoezi hili la ugawaji wa vitabu vya Kiada na Hadithi, hivyo waliomba Serikali ya awamu ya sita wakishrikiana na Halmashauri waendelee kusisitiza walimu watumie vitabu kwa usahihi kwa kuhakikisha wanafunzi wanahimizwa kuvitumia.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda