• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutembelea maendeleo ya Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

Posted on: November 30th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe.Ally Hapi amewataka Madiwani pamoja na wataalam kushirikiana kwa pamoja  katika kusimamia Miradi ya maendeleo inayotekelezwa  ili kufanikisha lengo la Serikali kutatua changamoto kwa waananchi,

Hayo amesema leo  Novemba 30,2021 baada ya kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne katika Shule ya Sekondari Makongoro na  Ujenzi wa vyumba viwili katika shule ya Msingi Shikizi Suguti zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mhe Hapi amesema kuwa kuna umuhimu wa  kila kiongozi kuwajibika kwa nafasi yake pamoja na kushirikiana  ili kuhakikisha  miradi inakamilika kwa wakati na viwango.

‘Msikae ofisini,muende maeneo ya mradi ili mkawasimamie mafundi vizuri,miradi ikamilike kwa wakati na viwango’.Amesema Mhe Hapi

Aidha Mhe Hapi amewataka viongozi  kutojiingiza katika vitendo vya rushwa kwa kutaka kupata  tenda  katika maeneo ya miradi kwani kanuni za utumishi haziruhusu.

‘kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi kutaka kupata tenda ya kusambaza vifaa katika maeneo ya miradi,ukifanya hivyo utaingia katika maslahi binafsi ni vyema ukaacha’’amesema Mhe Hapi

Mhe Hapi ametoa wito kwa  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kuwajengea uwezo vikundi vya Wanawake,Vijana na Watuwenyeulemavu ili waweze kuanzisha miradi ya vifaa vya ujenzi.

‘Tukiviwezesha vikundi  hivi Halmashauri pia itanufaika hasa katika miradi ya ujenzi’amesema Mhe.Hapi

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Joshua Nassari amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutembelea Wilaya ya Bunda na kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Mhe Nassari ameahidi kushirikiana na wakurugenzi wa halmashauri zote mbili ili kuhakikisha miradi inamalizika kwa wakati na Viwango.

‘Tunashukuru kwa Ujio wako Mhe Mkuu wa Mkoa,na niahidi tu sikuingine ukija utakuta miradi iko vizuri zaidi’’amesema Mhe Nassari

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bi.Changwa .Mkwazu awali akitoa taarifa ya ujenzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa amesema kuwa changamoto ambayo imefanya kuchelewa kuanza ujenzi ni kuchelewa kupatikana kwa vifaa ikiwa pamoja na vifaa kuchelewa kufika kwenye maeneo husika kutokana na changamoto ya barabara.

‘Kumekuwa na changamoto ya vifaa  hasa sementi,tunashukuru juhudi zimefanyika tumeanza kupeleka sementi katika maeneo mengi ya miradi’’Amesema Bi Mkwazu

Kwa hatua ingine Mhe.Hapi amesisitiza utulivu katika Mabaraza ya Madiwani kwakuhakikisha busara na hekima ina kuwepo katika kufanya maamuzi kwa masilahi ya Halmashauri.

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ilipokea fedha za mpango wa maendeleo kiasi chaTshs. 2,550,000,000 fedha kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya vyumba vya madarasa 67, ujenzi wa jengo la huduma za dharura,ujenzi wa jengo la ICU na Nyumba za Watumishi .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI June 04, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA YATOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MWIBARA

    June 04, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 03, 2025
  • ELIMU IENDELEE KUTOLEWA KWA VIJANA RIKA BALEHE.

    May 31, 2025
  • WAUGUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika:

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda