• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe.Joshua Nassari afungua mafunzo ya uhamasishaji wa kilimo cha zao la Pamba,aweka mkazo ili kufika malengo.

Posted on: November 16th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe Joshua Nassari  ametilia mkazo wa kuongeza tija ya  uhamasishaji wa  kilimo cha zao la pamba ili kuongeza tija katika zao hilo.

Mhe Nassri amesema hayo katika kikao cha uhamasishaji wa kilimo cha zao la pamba kilichofanya Novemba 16, 2021 katika ukumbi wa Malaika.

Mhe Nassari amesema kuwa ni wajibu wa viongozi wa Wilaya ya Bunda kusimamia kwa ukaribu shughuli za kilimo cha pamba ili kufanikisha malengo ya Wilaya kuzalisha Tani 50,000 katika msimu ujao wa  zao la pamba.

‘’Wataalam wa kilimo na viongozi wote mkasimamie ipasavyo ili kuweza kufikia lengo la Wilaya kuzalisha tani 50,000 na kuongeza tija katika zao hili’’alisema Mhe Nassari

Aidha Mhe.Nassari ametoa shukrani kwa balozi wa pamba Bwa.Aggrey Mwanri kwa kutoa mafunzo  kwa  Wataalam na Wakulima  wa Bunda.

‘Nina imani kupitia mafunzo haya,Bunda tutafanya vizuri zaidi’’.alisema Mhe. Nassari

Kwa upande wake, Balozi wa zao la pamba Bwa.Aggrey Mwanri amesema kuwa kilimo cha zao la pamba kinahitaji usimamizi na  kufuata kanuni bora ,ambazo zitamuwezesha mkulima  kuzalisha kwa tija.

‘’kwa kuzingatia matumizi ya mbolea,mbegu bora,kufuata vipimo vilivyopendekezwa na wataalam itasiadia kufikia malengo ya Wilaya,Mkoa na kitaifa katika zao la pamba’’alisema Bwa. Mwanri

Aidha Bwa. Mwanri ameeleza zaidi kuwa kilimo cha pamba kinaweza kubadilisha maisha ya Wananchi wa Bunda kiuchumi kama kutakua na mkakati madhubuti wa uzalishaji wenye tija.

‘Juhudi ziongezeke baada ya mafunzo haya ili kuvuna zaidi katika zao la pamba’.alisema Bwa.Mwanri

Awali  bwa.Mwanri alitaja kanuni mpya katika zao la pamba ni sentimita 60 mstari kwa mstari na sentimita 30 mche hadi mche lengo ikiwa kuzalisha kilo 300 hadi 1000 kwa hekari moja.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Bi.Changwa Mkwazu ametoa shukrani kwa balozi  wa Pamba  Bwa.Aggrey Mwanri kwakutoa elimu mpya juu ya uzalishaji pamba.

 ‘Awali wakulima walikua wanapata wastani wa kilo 300 badala ya 1000 ,kupitia mafunzo haya tunategemea mabadiliko makubwa’.alisema Bi Mkwazu

Aidha Bi.Mkwazu ameahidi kushirikiana na Wataalam wa kilimo, watendaji wa vijiji na viongozi wengine katika hatua ya upandaji,umwagiliaji wa dawa mpaka uvunaji.

‘ili kuhakikisha tunapata pamba iliyo bora  na inayokubalika katika soko’’alisema Bi.Mkwazu

Kampeni ya kuongeza tija ya uzalishaji wa kilimo cha zao la pamba itaendelea kufanyika ngazi ya vijiji na mtaa ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda itafanyika katika vijiji 78 na Halmashauri ya mji wa Bunda Mitaa 21.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda