• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA, APOKEA TAARIFA YA MAKABIDHIANO YA MRADI WA KUHIMILI ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI

Posted on: October 5th, 2023

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bunda, Bi. Changwa M. Mkwazu siku ya tarehe 4/10/2023 alipokea taarifa ya makabidhiano ya uratibu wa mradi wa kuhimili Athari za mabadiliko ya Tabianchi yaliyofanyika katika ofisi ya Mkurugenzi. Makabidhiano hayo yalifanyika baina ya ndugu Dickson Balige na ndugu Johanes Bucha.

Aliyekuwa Mratibu wa mradi ambaye anamaliza muda wake Ndugu Dickson Balige wakatika akikabidhi taarifa hiyo alisema, katika kipindi cha robo ya kwanza ya utekelezaji wa mradi, shughuli mbalimbali zimeanza kutekelezwa katika sekta ya maji, kilimo, ufugaji wa samaki na mazingira.  

“Katika kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi mradi umeanza kusambaza maji kwa jamii kwa kuongeza mtandao wa maji katika vijiji vya Mumagunga na Muranda, kuanzisha na kuimarisha jumuiya za watumia maji (CBWOSOs) katika vijiji vya Muranda, Mwiruma, Mumagunga na Kibara”. Alisema Ndugu Balige.

Pia kwa upande wa kilimo mradi umelenga kuboresha maisha ya wakulima walioathiriwa na mabadiliko ya Tabianchi kwa kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula kwa kutumia kilimo kinachozingatia hifadhi ya mazingira.

“Kwa upande wa ufugaji wa samaki mradi huu umelenga kuhamasisha uvuvi endelevu katika halmashauri kwa kuanzisha ufugaji wa samaki kupitia mabwawa na vizimba katika vikundi vya ufugaji wa samaki ili kuboresha maisha na kuhimili athari za mabadiliko ya Tabianchi katika vijiji vya Mchigondo na Isanju. Kupitia mradi huu tumeweza kununua mitumbwi miwili na injini mbili za HP-15 kwa ajili ya utoaji wa huduma katika vizimba vya kufugia samaki”. Alisema aliyekuwa Mratibu wa mradi.

Ndugu Balige alisema, katika kuboresha mazingira na ikolojia kwa kuzingatia shughuli zinazoimarisha maisha ya jamii za vijiji vilivyoathiriwa na mabadiliko ya Tabianchi, kwa kuanzisha kitalu na upandaji wa miti katika vilima vipara vya Kata za Iramba, Neruma, Namhula, Chitengule na Igundu. Kupitia mradi huu tuliweza kupanda miche 159,030, ambapo miche 63,500 imepandwa katika taasisi mbalimbali za serikali na binafsi na miche 95,530 inaendelea kukuzwa katika kitalu.

Halmashauri iliandika kiushindani andiko la mradi huu ambao ulikidhi vigezo na kupitishwa na bodi ya mfuko wa mazingira duniani mnamo mwezi April, 2021 likiwa na thamani ya dola za Kimarekani 1,400,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za mradi kwa kipindi cha miaka mitatu.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda