• Malalamiko |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
Bunda District Council
Bunda District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji & Ushirika
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maji
      • Fedha & Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Mifugo & Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Rasilimali Watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi & Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Elimu Msingi
    • Barabara
    • Mifugo
    • Afya
    • Mazao ya kilimo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi & Mipango
      • Elimu, Afya & Maji
      • AIDS Control
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Uma
    • Video
    • Hifadhi ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YA SIASA YA WILAYA IMEUPONGEZA UONGOZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA KWA USIMAMIZI MZURI WA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MARA

Posted on: May 17th, 2024

Kamati ya siasa ya Wilaya ya Bunda ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama (CCM) Ndugu Mayaya A. Magesse imeupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa usimamizi wao mzuri katika mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana Mara, iliyopo katika kijiji cha Bulamba Kata ya Butimba.

Pongezi hizo zilitolewa na kamati ya siasa ya Wilaya ya Bunda walipofanya ziara siku ya tarehe 16/5/2024 ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo.

Wajumbe wa kamati ya siasa walitembelea na kukagua jengo moja baada ya lingine, ikiwemo na miundombinu yote iliyopo katika shule hiyo ya wasichana Mara ambapo walimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Bunda, pamoja na uongozi mzima wa Halmashauri kwa usimamizi wao mzuri.


Katika ziara hiyo, wajumbe walishauri ulinzi katika eneo hilo uongezwe na kuhakikisha wanajenga uzio mapema ili kuzuia masuala ya wizi na kulinda mali zote zilizopo eneo la mradi.

Kamati pia, walishauri Halmashauri ihakikishe wanachimba kisima cha kuhifadhi maji, na kuhakikisha wananunua matanki kwa ajili ya kuvunia maji ya mvua badala ya kutegemea maji ya bomba pekee, pia, walishauri zifungwe solar katika shule hiyo ambapo zitasaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa eneo hilo pale umeme wa TANESCO utakapokuwa umekatika.

Ndugu Magesse alimshukuru Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali kujenga mradi huu mahali hapa na alisisitiza suala la kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha changamoto zote zilizobainishwa na wajumbe wa kamati zinarekebishwa na aliwataka wananchi kuwa walinzi wa shule pamoja na miundombinu yote iliyopo katika eneo hilo la mradi, kwani wao ndio wanufaika wakuu katika mradi huo.

“Endeleeni kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na msikate tamaa katika kusimamia miradi mingine ya maendeleo na mfanyekazi kwa bidii.” Alisema Ndugu Magesse.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mh. Dkt. Vicent Anney alisema ulinzi wa eneo hilo kwa sasa umeimarishwa zaidi tofauti na hapo awali, na alimuhakikishia Mwenyekiti wa kamati kuwa kazi zinafanyika vizuri na Halmashauri inasimamia vizuri mradi huo kwa kuhakikisha unajengwa kwa viwango sahihi na kukamilika kwa wakati.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI KWA NAFASI ZA UDEREVA May 07, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO September 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 18, 2024
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 20, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI

    April 26, 2025
  • WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU 5 YA UANDAAJI NA UTENGENEZAJI WA MPANGO MKAKATI

    April 25, 2025
  • PROJECT ZAWADI YAIPIGA TAFU MASHINDANO YA UMITASHUMTA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA

    April 07, 2025
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUNDA WAPEWA TUZO NA ZAWADI .

    April 03, 2025
  • Angalia zote

Video

Mvamizi wa eneo la soko.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Baraza la Madiwani
  • Dira na Dhamira
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Mpango Mkakati
  • Mpango wa Uwekezaji Sekta ya Samaki
  • Muundo wa Taasisi
  • OPRAS - Form

Viunganishi Muambata

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2023 Bundadc
  • Matokeo ya darasa la saba
  • Matokeo ya darasa la saba
  • PO-RALG
  • PO-PSM
  • Matokeo ya Kidato cha Nne 2019

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Kibara Stoo.

    Anuani ya Posta: 126, Bunda

    Simu: 0282621055

    Hamishika: 0742163056

    Barua Pepe: ded@bundadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki@ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bunda